Evangelistic Assemblies Of God Tanzania (E.A.G.T MKIMBIZI BIMA)
BIBLIA INATUFUNDISHA NINI ❓ Mawasiliano 0755844288/0688964004 SOMO ; Jinsi NDOA Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha MUNGU anataka familia (katika NDOA) ziwe na hali gani❓ 1 👈👉MUNGU alianzisha ndoa ya kwanza. Biblia inasema kwamba alimuumba mwanamke wa kwanza na “akamleta kwa mwanamume.” Adamu alifurahi sana, naye akasema hivi: “Hatimaye huyu ni mfupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu.” (Mwanzo 2:22, 23) Jambo hilo linaonyesha kwamba MUNGU anataka wale waliofunga ndoa wawe na furaha. 2 👈👉Cha kusikitisha, leo familia nyingi hazina furaha. Hata hivyo, Biblia ina maagizo yanayozoweza kumsaidia kila mtu katika familia atimize majukumu yake na kufurahia kuwa pamoja.—Luka 11:28 ,"LAKINI YEYE ALISEMA, AFADHALI, HERI WALISIKAO NENO LA MUNGU NA KULISHIKA ." MUNGU ANATARAJIA WAUME WAFANYE NINI? 3, 4. (a) Mume anapaswa kumtendeaje mke wake❓ (b) Kwa nini ni muhimu kwa mume na mke kusameheana kwa hiari❓ 3 Biblia inasema kwamba mume mzuri anapaswa kumpenda na kumheshimu